Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 267 2026-05-07

Name

Arif Suleiman Premji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ARIF S. PREMJI aliuliza:-

Je, Shule ngapi za kidato cha tano na sita zimejengwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 hadi kufikia robo ya pili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Arif Suleiman Premji, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikijenga shule mpya za kidato cha tano na sita au kuongeza miundombinu katika shule za sekondari zilizopo ili kuzipandisha hadhi, kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita, kisha kupata usajili rasmi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imetoa shilingi billioni 23.8 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 318, mabweni 116, matundu ya vyoo 542 katika shule 68 za sekondari ili kuziongezea uwezo wa kupokea wanafunzi wa kidato cha tano na sita. Aidha, hadi Aprili, 2026 shule 80 zenye uwezo wa kupokea wanafunzi 6,400 wa kidato cha tano na sita zimesajiliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali imetenga shilingi billioni 27.5 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 273, madarsa 1,094 na matundu ya vyoo 1,645 katika shule 91 za sekondari kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita. Ahsante.