Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 11 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 120 | 2026-04-17 |
Name
Amosy William Maganga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Primary Question
MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha SGR katika eneo la Nyahuwa ili kuboresha usafiri na usafirishaji?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Amosy Maganga kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza (kilometa 1,219), Tabora hadi Kigoma (kilometa 506) na Uvinza hadi Musongati (kilometa 282). Aidha, ujenzi wa reli ya kisasa kuanzia Makutupora hadi Tabora (SGR Lot 3) unaendelea kutekelezwa ambapo eneo la Nyahuwa linapatikana katika kipande hiki cha ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa tathmini na usanifu uliofanyika, kipande cha tatu cha kutoka Makutupora hadi Tabora kitakuwa na Kituo Kikuu kwa ajili ya abiria na mizigo katika Mji wa Tabora. Vituo vya kati katika Mji wa Manyoni na Itigi na vituo vidogo kwa ajili ya abiria pekee kwenye Mji wa Tura, Malongwe, Goweko na Igalula. Aidha, Katika Mji wa Nyahuwa, itajengwa njia ya kuchepushia treni (passing loop). Wakazi wa Mji wa Nyahuwa wataendelea kupata huduma za SGR katika vituo vilivyo karibu, yaani Malongwe na Goweko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maamuzi ya maeneo ya kuwekwa kwa vituo vya abiria na mizigo vya aina mbalimbali hufanywa kupitia upembuzi yakinifu uliofanywa kwa kuzingatia mahitaji ya kiuchumi, biashara na kijamii kwa miji na vijiji vyote vilivyopo pembezoni mwa reli, pamoja na kuzingatia umbali baina ya kituo cha mwendokasi kwa treni ya SGR ili kuweza kuendeshwa kwa tija na ufanisi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved