Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 11 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 118 | 2026-04-17 |
Name
Shaffin Ahmedali Sumar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uyui
Primary Question
MHE. SHAFFIN A. SUMAR aliuliza: -
Je, lini Serikali itafanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Bwawa la Maji na Chujio katika Kata ya Shitage?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Shaffin Ahmedali Sumar, Mbunge wa Jimbo la Uyui, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Bwawa la Maji la Shitage katika Kijiji cha Shitage Kata ya Shitage Wilayani Uyui Mkoa wa Tabora. Mara baada ya ujenzi wa bwawa hilo kukamilika, usanifu wa miundombinu ya usambazaji maji ukijumuisha mtambo wa kuchuja na kutibu maji utafanyika. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved