Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 11 Water and Irrigation Wizara ya Maji 118 2026-04-17

Name

Shaffin Ahmedali Sumar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uyui

Primary Question

MHE. SHAFFIN A. SUMAR aliuliza: -

Je, lini Serikali itafanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Bwawa la Maji na Chujio katika Kata ya Shitage?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Shaffin Ahmedali Sumar, Mbunge wa Jimbo la Uyui, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Bwawa la Maji la Shitage katika Kijiji cha Shitage Kata ya Shitage Wilayani Uyui Mkoa wa Tabora. Mara baada ya ujenzi wa bwawa hilo kukamilika, usanifu wa miundombinu ya usambazaji maji ukijumuisha mtambo wa kuchuja na kutibu maji utafanyika. Ninakushukuru.