Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 58 2026-04-10

Name

Kijakazi Mohamed Yunus

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KIJAKAZI Y. MOHAMED aliuliza: -

Je, lini Mkataba wa kuchakata Gesi Asilia (LNG) Lindi utasainiwa na kuanza utekelezaji?

Name

Salome Wyckiffe Makamba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kijakazi Yunus Mohamed, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali na wawekezaji wa mradi wa kuchakata gesi asilia (LNG) Mkoani Lindi wapo katika hatua ya mwisho ya majadiliano, hususan kwenye masuala ya kisheria ili kuwezesha usainishaji wa mikataba na makubaliano, na hatimaye utekelezaji wa mradi kuanza. Aidha, wabia wa mradi wameendelea na miradi ya kijamii ikiwemo ujenzi wa Shule ya Msingi Mpya ya Likong’o ambayo ujenzi wake umefikia 90%.