Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 57 2026-04-10

Name

Happiness Daniel Ngwando

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAPPINESS D. NGWANDO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za usalama mipakani ili kuwezesha vyombo vya ulinzi na usalama kufanya doria?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Happiness Daniel Ngwando, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara za usalama mipakani ni barabara zinazoambaa na mipaka ya nchi yetu kwa ajili ya kuwezesha vyombo vya usalama kuimarisha ulinzi na usalama mipakani. Kwa kutambua umuhimu wa barabara hizi, Serikali inaendelea kuzijenga kwa kiwango cha changarawe ili ziweze kutumika na vyombo vya usalama kufanya doria mipakani.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa Serikali kupitia TANROADS imejenga jumla ya kilometa 1,759 kwa kiwango cha changarawe katika Mikoa ya mipakani. Aidha, Serikali inaendelea kujenga sehemu zilizobaki kwa awamu kwa kiwango cha changarawe kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.