Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 57 | 2026-04-10 |
Name
Happiness Daniel Ngwando
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HAPPINESS D. NGWANDO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za usalama mipakani ili kuwezesha vyombo vya ulinzi na usalama kufanya doria?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Happiness Daniel Ngwando, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, barabara za usalama mipakani ni barabara zinazoambaa na mipaka ya nchi yetu kwa ajili ya kuwezesha vyombo vya usalama kuimarisha ulinzi na usalama mipakani. Kwa kutambua umuhimu wa barabara hizi, Serikali inaendelea kuzijenga kwa kiwango cha changarawe ili ziweze kutumika na vyombo vya usalama kufanya doria mipakani.
Mheshimiwa Spika, hadi sasa Serikali kupitia TANROADS imejenga jumla ya kilometa 1,759 kwa kiwango cha changarawe katika Mikoa ya mipakani. Aidha, Serikali inaendelea kujenga sehemu zilizobaki kwa awamu kwa kiwango cha changarawe kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved