Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 55 2026-04-10

Name

Kija Limbu Ntemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katoro

Primary Question

MHE. KIJA L. NTEMI aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Zimamoto ili kusaidia majanga ya moto yanapotokea Katoro?

Name

Kaspar Kaspar Mmuya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali Na. 55 la Mheshimiwa Injinia Kija Limbu Ntemi, Mbunge wa Katoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kusogeza huduma za zimamoto na uokoaji karibu na wananchi ikiwemo ujenzi wa vituo vya zimamoto na uokoaji. Aidha, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limepata kiwanja Na. 1384 kilichopo Kitalu Namba “A” chenye ukubwa wa mita za mraba 4,987 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Zimamoto na Uokoaji katika Mji wa Katoro, na utaratibu wa kupata hatimiliki zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.