Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 54 2026-04-10

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, Serikali inachukua hatua gani kuwawezesha Wananchi hususan Vijana na Wavuvi wadogo kushiriki kikamilifu katika uchumi wa buluu?

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ya kuwawezesha wananchi, hususan vijana na wavuvi wadogo, kushiriki kikamilifu katika uchumi wa bluu kwa lengo la kuongeza ajira, kipato, na mchango wa sekta ya uvuvi katika uchumi wa Taifa. Serikali inaendelea kutekeleza Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora, ambapo katika mwaka wa fedha 2025/2026 Wizara imepokea kiasi cha shilingi bilioni 30.7 (shilingi bilioni 25.9 katika Uvuvi na shilingi bilioni 4.75 katika Mifugo), kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi wadogo pamoja na vijana katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, aidha, kupitia Programu hii ya BBT, vijana 308 kutoka mikoa yote nchi nzima wamepatiwa mikopo isiyo na riba na yenye masharti nafuu kwa ajili ya kutekeza miradi ya ufugaji wa samaki kwenye vizimba, ufugaji wa majongoo bahari, unenepeshaji kaa na kilimo cha mwani.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inaendelea kutekeleza zoezi la utoaji wa mikopo isiyo na riba na yenye masharti nafuu kwa wavuvi wadogo, wakiwemo vijana, kwa kuwawezesha kupata nyenzo za uvuvi ikiwemo maboti ya kisasa pamoja na nyavu za uvuvi.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.