Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 6 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Uchukuzi | 52 | 2026-04-10 |
Name
Mwanaisha Ng'anzi Ulenge
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -
Je, lini Serikali itatwaa maeneo ya karibu na Bandari ya Tanga, ili kuongeza eneo la utekelezaji wa shughuli za Bandari?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa Mnyaa, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ulenge, Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Tanga, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa eneo katika Bandari ya Tanga, Serikali kupitia TPA, inaendelea na taratibu za utwaaji wa eneo karibu na Lango Namba Mbili na eneo la Police Marine, ili yatumike kwa ajili ya shughuli za kibandari.
Mheshimiwa Spika, pamoja na utwaaji wa maeneo hayo, TPA inaendelea na mpango wa matumizi bora ya maeneo yaliyopo ndani ya bandari, ikiwa ni pamoja na uhamishaji wa baadhi ya maghala, ili kuongeza maeneo ya kufanyia shughuli za kibandari.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved