Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 6 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 50 | 2026-04-10 |
Name
Zuena Athumani Bushiri
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga chanzo cha maji kilichobebwa na mafuriko katika Kata ya Maore Same Mashariki?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika mpango wa muda mfupi, Serikali kwa kushirikiana na wananchi wa Kata ya Maore imekamilisha ukarabati wa dharura wa chanzo cha maji Maore na sasa zaidi ya wananchi 14,000 wa vijiji vitatu vya Maore, Kadandu na Mheza vinavyopatikana katika kata hiyo, wanapata huduma ya majisafi na salama.
Mheshimiwa Spika, katika mpango wa muda mrefu, Serikali inaendelea na usanifu wa mradi utakaojumuisha pia maboresho ya ujenzi wa chanzo cha Maore. Usanifu wa mradi huo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2025/2026 na utekelezaji wake kufanyika baada ya fedha kupatikana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved