Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 47 2026-04-10

Name

Emanuel Qambaji Nuwas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. EMANUEL Q. NUWAS aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kuongeza muda wa marejesho ya Mikopo ya asilimia mbili kwa Watu wenye Ulemavu ili kujenga usawa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Mwongozo wa utoaji, usimamizi na urejeshaji wa fedha za mikopo ya 10% kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, hakuna ukomo au muda maalum wa marejesho uliowekwa.

Mheshimiwa Spika, muda na utaratibu wa marejesho kwa makundi yote ikiwemo kundi la watu wenye ulemavu hufuata makubaliano kati ya halmashauri na wakopaji kwa kuzingatia aina ya miradi na aina ya mtiririko wa fedha katika shughuli iliyoombewa mkopo ili kuongeza ufanisi wa shughuli za wajasiriamali na marejesho ya mikopo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kusimamia Sheria, Kanuni na Miongozo ili kuwezesha makundi haya kunufaika na fursa hizi za mikopo ya 10%, ahsante.