Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 154 2026-04-21

Name

Mecktridis Fratern Mdaku

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA K.n.y. MHE. MECKTRIDIS F. MDAKU aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Ifakara – Lupilo hadi Malinyi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mecktridis Fratern Mdaku, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Ifakara – Lupilo hadi Malinyi kwa kiwango cha lami kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huu ilikuwa ni kukamilisha ujenzi wa daraja la Magufuli (meta 384) katika Mto Kilombero pamoja na barabara ya maingilio (kilometa 9.143) ambalo lilikuwa kikwazo kikubwa katika barabara hii.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa, Serikali imesaini mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Ifakara – Lupilo – Mtimbira yenye urefu wa kilometa 112 ambapo taratibu za malipo ya awali kwa Mkandarasi ili aweze kuanza kazi zinaendelea. Kwa sehemu zilizobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi.