Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Water and Irrigation Wizara ya Maji 151 2026-04-21

Name

Benjamin Lukubha Ngayiwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Primary Question

MHE. BENJAMIN L. NGAYIWA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa chujio la maji la Buzwagi na tenki la maji la Shunu/Lugela ili kupunguza kero ya kukatika kwa maji Kahama?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Benjamin Lukubha Ngayiwa, Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi inaendelea na mradi wa ujenzi wa mtambo wa kutibu na kusafisha maji (treatment plant) katika eneo la Buzwagi Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga. Utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 79% na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2026.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji Lugela unaojumuisha ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita 75,000 katika eneo la Lugela Kata ya Nyahanga wilayani humo. Kazi nyingine zinazotekelezwa ni pamoja na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa tisa ambapo umeanza kutoa huduma kwenye baadhi ya maeneo ya Lugela.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa mradi huo umefikia wastani wa 78% za utekelezaji na unatarajiwa kukamilika Juni, 2026 na kunufaisha wananchi wapatao 2,682 wanaoishi katika eneo la Lugela.