Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 13 Water and Irrigation Wizara ya Maji 150 2026-04-21

Name

Thomas Maganga Kampala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. THOMAS K. MAGANGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha malipo ya mkandarasi wa Mradi wa Bwawa la Nsekwa ili akamilishe kazi hiyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Thomas Kampala Maganga, Mbunge wa Jimbo la Katavi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kufuatia ujenzi wa Bwawa la Nsekwa kufikia hatua nzuri, Serikali inaendelea na ujenzi wa mradi wa miundombinu ya kutibu na kusafisha maji yanayotokana na bwawa hilo lililopo Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi. Utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 10% na unatarajia kuwanufaisha zaidi ya wananchi 68,426 waishio katika vijiji 16 vya Wilaya ya Mlele.

Mheshimiwa Spika, mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 1.5, ambapo tayari Serikali imelipa fedha za malipo ya awali (advance payment) kiasi cha shilingi 226.5 kwa mkandarasi na yupo eneo la kazi akiendelea na utekelezaji wa mradi.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kupeleka fedha za utekelezaji wa mradi huo kadiri hati za madai zitakavyowasilishwa ili kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi.