Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 13 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 149 | 2026-04-21 |
Name
Yohana Stephen Msita
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Itigi
Primary Question
MHE. YOHANA S. MSITA aliuliza: -
Je, upi mpango wa Serikali wa kuondoa kero ya wanyama waharibifu kama tembo kwenye Jimbo la Itigi?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Yohana Msita, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu katika Jimbo la Itigi, ikiwemo kuendelea kutumia kituo cha kudumu cha Askari kilichopo katika Kijiji cha Doroto na kambi za muda mfupi tatu kwenye Vijiji vya Chisingisa, Sanjaranda, na Kitaraka kwa ajili ya kuitikia kwa haraka kwenye matukio na kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu, kuendelea na kuimarisha doria za kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu; kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu mbinu rafiki za kudhibiti wanyamapori hao; kuendelea kugawa nyenzo na vifaa rafiki kwa wananchi ili kudhibiti na kuzuia wanyama waharibifu hao, tembo, kwa vijiji mbalimbali; kuendelea kutumia teknolojia ya ndege nyuki; na kuendelea kushirikiana na wadau.
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la Southern Tanzania Elephant Program (STEP) imetengeneza vihenge 24 vya kuhifadhi mazao yaliyoboreshwa. Sambamba na hatua hizo, Serikali imevuna tembo wawili waliokuwa wakihatarisha usalama wa maisha na mali za wananchi katika Vijiji vya Doroto na Sanjaranda.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved