Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 13 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 144 | 2026-04-21 |
Name
Prof. Joyce Lazaro Ndalichako
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kasulu Mjini
Primary Question
MHE. PROF. JOYCE L. NDALICHAKO aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Kasulu – Kigondo na Habitat – Hwazi, kupitia Mradi wa TACTIC?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Joyce Lazaro Ndalichako, Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Kasulu ni miongoni mwa halmashauri za miji 45 inayotekeleza Mradi wa TACTIC nchini. Mji wa Kasulu uko kundi la tatu la utekelezaji wa Mradi wa TACTIC lenye miji 18. Katika mradi huu, Halmashauri ya Mji wa Kasulu imetengewa shilingi billioni 10.87.
Mheshimiwa Spika, Mradi wa TACTIC umekamilisha usanifu wa miradi ya Mji wa Kasulu wa Barabara za Makaburi – Kigondo, kilometa 3.77, Habitat – Hwazi, km 2.04, jumla ya kilometa 5.8. Mradi huu unahusisha pia ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Murus na Soko la Kumsenga, Kasulu. Baada ya kukamilisha usanifu wa miradi hii yote, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inaendelea na taratibu za maandalizi ya kuanza utekelezaji wa miradi katika kundi hili, ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Kasulu. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved