Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 28 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Mifugo 534 2025-05-20

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. SAPUTU aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati Mnada wa Olokii uliopo Kata ya Bwawani – Arumeru Magharibi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inawajibu wa kuhakikisha kuwa biashara ya mifugo inafanyika katika mazingira yenye miundombinu muhimu ili kurahisisha biashara hiyo. Aidha, Mnada wa Olokii uliopo katika Kata ya Bwawani, Arumeru Magharibi ni mnada wa upili unaosimamiwa moja kwa moja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi na mnada huu hufanya kazi kila Ijumaa ya wiki.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ukarabati wa mnada huo Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ipo katika taratibu za umiliki wa eneo la mnada huo na mara tu taratibu hizo zitakapokamilika Serikali itakua tayari kufanya ukarabati wa mnada huo.