Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 28 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 353 2025-05-20

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. MOHAMMED JUMAH SOUD aliuliza: -

Je, kwa nini NEMC haianzishi utaratibu wa kuishirikisha ZEMA ili kuongeza ufanisi wa uibuaji na usimamizi wa miradi ya mazingira Zanzibar?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ili kuongeza ufanisi katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumekuwa na utaratibu wa kushirikiana kati ya NEMC na ZEMA katika uibuaji na usimamizi wa miradi ya mazingira. Miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali zikiwemo hatua za maandalizi na utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa mradi unaotekelezwa ni mradi wa kuimarisha uwezo wa jamii za pwani kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Mradi huu unatekelezwa Unguja na Pemba kwa thamani ya dola za Kimarekani milioni moja. Aidha, miradi miwili inayoandaliwa kwa ushirikiano wa NEMC na ZEMA ni kama ifuatavyo: -

(a) Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo yenye upungufu wa maji baridi; mradi huu upo katika hatua za kupata kibali cha fedha kutoka Mfuko wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi - Adaptation Fund na utatekelezwa Unguja na Pemba kwa thamani ya dola za Kimarekani milioni 3.5.

(b) Mradi wa kuimarisha miundombinu katika ukanda wa pwani ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi; mradi huu upo katika hatua za kupitishwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika na utatekelezwa Tanzania Bara na Zanzibar, nakushukuru.