Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 28 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 351 | 2025-05-20 |
Name
Dr. Pius Stephen Chaya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Manyoni
Primary Question
MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:-
Je, kuna mpango gani wa kurasimisha viongozi wa nyumba kumi (mabalozi) kama sehemu ya kuimarisha usalama wa raia?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa ulinzi na usalama katika ngazi ya msingi kwa maendeleo ya Taifa. Aidha, usalama wa raia umeendelea kusimamiwa na vyombo vya usalama kwa kushirikiana na wananchi kupitia mfumo wa uongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika ngazi za msingi ikiwemo Wenyeviti wa Vijiji/Mitaa, Vitongoji na Mabalozi. Serikali itaendelea kuboresha mfumo wa utambuzi na usalama katika ngazi ya msingi kwa kupitia mfumo wa uongozi wa Serikali za Mitaa uliopo ili kuongeza ufanisi katika kuimarisha masuala ya usalama, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved