Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 351 2025-05-20

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kurasimisha viongozi wa nyumba kumi (mabalozi) kama sehemu ya kuimarisha usalama wa raia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa ulinzi na usalama katika ngazi ya msingi kwa maendeleo ya Taifa. Aidha, usalama wa raia umeendelea kusimamiwa na vyombo vya usalama kwa kushirikiana na wananchi kupitia mfumo wa uongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika ngazi za msingi ikiwemo Wenyeviti wa Vijiji/Mitaa, Vitongoji na Mabalozi. Serikali itaendelea kuboresha mfumo wa utambuzi na usalama katika ngazi ya msingi kwa kupitia mfumo wa uongozi wa Serikali za Mitaa uliopo ili kuongeza ufanisi katika kuimarisha masuala ya usalama, ahsante.