Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 9 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 102 | 2026-04-15 |
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza: -
Je, lini ujenzi wa Makao Makuu ya TANAPA Kanda ya Magharibi utaanza?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) linasimamia Hifadhi za Taifa 21 zilizogawanywa katika Kanda Nne, ikiwemo Kanda ya Magharibi, ambayo Makao Makuu yake yapo Mji wa Bunda, Mkoa wa Mara. Kanda hii inajumuisha Hifadhi za Taifa zipatazo tisa zinazosimamiwa na TANAPA, ikiwemo Hifadhi za Taifa Serengeti, Visiwa vya Saanane na Rubondo, Burigi - Chato, Milima Mahale, Ibanda - Kyerwa, Rumanyika - Karagwe, Mto Ugalla na Gombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali imetenga eneo lenye ukubwa wa ekari 41.13 katika eneo la Kata ya Balili, Bunda Mjini, kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Kanda ya Magharibi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Wizara kupitia TANAPA imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizo. Aidha, taratibu zote za maandalizi za kuanza ujenzi wa mradi huo, ikiwemo usanifu wa majengo na gharama za ujenzi wa mradi huo, zimekamilika. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved