Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 9 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 97 2026-04-15

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Barabara ya Uyole - Nsalaga - Ifisi mpaka Uwanja wa Ndege Songwe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Uyole kuanzia pale Nsalaga hadi Ifisi yenye urefu wa kilometa 26 kwa njia nne unaendelea, na umefikia 41.7%. Mradi huu unatarajiwa kukamilika tarehe 23 Januari, 2027. Kwa sehemu iliyobaki ya Ifisi hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe ambayo ina urefu wa kilometa 3.7, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kujenga hicho kipande ambacho kitakuwa kimesalia.