Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 9 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 96 | 2026-04-15 |
Name
Subira Khamis Mgalu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara ya Tamko - Mapinga kwa kipande kilichosalia?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Barabara ya TAMCO – Mapinga unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza inahusisha sehemu ya kuanzia NIDA hadi Pangani kilometa 3.8 na awamu ya pili inahusisha sehemu ya Pangani hadi Mapinga kilometa 14.62.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara hii unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2027. Aidha, Serikali inaahidi kuipa kipaumbele barabara hii kama sehemu ya kupunguza msongamano kwenye barabara kuu ya Dar es Salaam – Morogoro. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved