Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 91 2026-04-15

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESTA L. KAIZA aliuliza: -

Je, nini msimamo wa Serikali kuhusu suala la Wazazi kuchangia Mitihani, Masomo ya Ziada na Chakula Shule za Msingi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnesta Lambert Kaiza, Mbunge wa Jimbo la Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2016 Serikali ilianza utekelezaji wa Elimu Msingi bila ada kupitia Waraka wa Elimu Namba Tatu wa mwaka 2016. Waraka huu pamoja na mambo mengine, unabainisha majukumu ya mzazi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa mtoto anapata vifaa vya kujifunzia, sare za shule, chakula na huduma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ajili ya kuboresha ujifunzaji na ufundishaji ikiwa ni pamoja na ustawi wa wanafunzi, Kamati na Bodi za Shule kupitia vikao vya wazazi zimekuwa zikianzisha michango mbalimbali. Ili kudhibiti michango holela, Serikali imekuwa ikiwaelekeza viongozi wa Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa michango ya aina yoyote inaridhiwa kupitia vikao rasmi vya wazazi na kamati au bodi za shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kwa wanafunzi wa bweni, Serikali imeweka katika fomu za maelekezo ya kujiunga (joining instructions) mahitaji na michango muhimu ambayo mwanafunzi anatakiwa kwenda nayo shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikifuatilia kuhakikisha kuwa hakuna michango holela; na kiongozi au mwalimu yeyote anayebainika kuanzisha michango iliyo kinyume na utaratibu, hatua za kinidhamu na za kiutawala zimekuwa zikichukuliwa. Ahsante.