Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 89 2026-04-15

Name

Fadhili Fabian Ngajilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. FADHILI F. NGAJILO aliuliza: -

Je, lini Soko la Machinga Complex Iringa litaanza kujengwa kama alivyoahidi Mheshimiwa Rais kwenye Kampeni za Mwaka 2025?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Fadhili Fabian Ngajilo, Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa ujenzi wa Soko la Machinga ulibuniwa na Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mwaka wa fedha 2024/2025 ili kukabiliana na changamoto inayowakabili wafanyabiashara wadogo na wa kati, hususan ukosefu wa maeneo sahihi ya kufanyia biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu utajengwa katika eneo la stendi ya mabasi ya zamani lenye ukubwa wa meta za mraba 6,505 lililopo Mtaa wa Stendi Kuu, Kata ya Kitanzini, kwa gharama ya shilingi bilioni 4.67. Soko litakalojengwa litakuwa na vizimba 800, maduka 150 na migahawa nane vyenye uwezo wa kuchukua wafanyabiashara 958 ambapo kati yao wafanyabiashara wadogo 800, wafanyabiashara wa kati 150 na mama na baba lishe wanane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imetenga kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi, ahsante.