Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 89 | 2026-04-15 |
Name
Fadhili Fabian Ngajilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iringa Mjini
Primary Question
MHE. FADHILI F. NGAJILO aliuliza: -
Je, lini Soko la Machinga Complex Iringa litaanza kujengwa kama alivyoahidi Mheshimiwa Rais kwenye Kampeni za Mwaka 2025?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Fadhili Fabian Ngajilo, Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa ujenzi wa Soko la Machinga ulibuniwa na Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mwaka wa fedha 2024/2025 ili kukabiliana na changamoto inayowakabili wafanyabiashara wadogo na wa kati, hususan ukosefu wa maeneo sahihi ya kufanyia biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu utajengwa katika eneo la stendi ya mabasi ya zamani lenye ukubwa wa meta za mraba 6,505 lililopo Mtaa wa Stendi Kuu, Kata ya Kitanzini, kwa gharama ya shilingi bilioni 4.67. Soko litakalojengwa litakuwa na vizimba 800, maduka 150 na migahawa nane vyenye uwezo wa kuchukua wafanyabiashara 958 ambapo kati yao wafanyabiashara wadogo 800, wafanyabiashara wa kati 150 na mama na baba lishe wanane.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imetenga kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved