Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 26 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Waziri wa Mifugo na Uvuvi | 338 | 2025-05-16 |
Name
Miraji Jumanne Mtaturu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mashariki
Primary Question
MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga majosho ya kuogeshea mifugo kwenye vijiji vya Jimbo la Singida Mashariki?
Name
Alexander Pastory Mnyeti
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Misungwi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2022/2023 Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilitumia kiasi cha shilingi milioni 92 kwa ajili ya kujenga majosho manne katika Halmashauri ya Ikungi linapopatikana Jimbo la Singida Mashariki ambapo kupitia fedha hizo Jimbo la Singida Mashariki lilifanikiwa kujengewa josho moja lililopo katika Kijiji cha Ntuntu lenye thamani ya shilingi milioni 23. Josho hilo limekamilika kwa 100% na linafanya kazi. Aidha, Wizara inaendelea kuratibu ujenzi wa majosho katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo vijiji vya Jimbo la Singida Mashariki kadiri ya upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Spika, aidha, Wizara inashauri Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi inayosimamia Jimbo la Singida Mashariki kutenga fedha kutoka katika mapato yao ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa majosho katika jimbo hilo kwa lengo la kudhibiti magonjwa yaenezwayo na kupe, mbung’o na wadudu wengine, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved