Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 26 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 332 2025-05-16

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kakonko

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapandisha madaraja kwa mserereko walimu wenye changamoto ya kupandishwa madaraja wakiwemo walimu wa Kakonko?

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu cha 6(1)(b) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura, 298 jukumu la kuwapandisha vyeo watumishi ni la mwajiri husika. Jukumu hili hutekekelezwa baada ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kutoa mwongozo kuwataka waajiri kuandaa na kuwasilisha ikama na bajeti ya mwaka husika wa fedha na Ofisi kuridhia utekekelezaji wa bajeti hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2024/2025 Serikali imetoa mwongozo unaohusu upandishwaji vyeo na ubadilishaji kada ikiwemo na kwa watumishi waliocheleweshwa kupandishwa vyeo. Hivyo, nitoe wito kwa waajiri wote nchini kutekeleza kwa wakati mwongozo huo ili kuepusha malalamiko kwa watumishi wa umma wenye changamoto za kupandishwa vyeo wakiwemo watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko.