Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 331 2025-05-16

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:-

Je, lini Serikali itazipandisha hadhi Barabara ya Isenyela - Sangambi - Lupa - Lualaje na Chunya Godima - Sangambi kuwa chini ya TANROADS?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, suala la kupandisha hadhi barabara ni la kisheria kwakuzingatia vigezo vilivyowekwa. Ikiwa kuna barabara ambayo inakidhi vigezo kutoka daraja la barabara ya wilaya kwenda daraja la barabara ya mkoa inatakiwa barabara hiyo ijadiliwe kwenye Kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa husika na ikionekana inakidhi vigezo ndipo bodi hiyo kupitia Mwenyekiti itamshauri Waziri mwenye dhamana na barabara kuwa barabara husika imekidhi vigezo vya kuwa na hadhi ya barabara ya mkoa na hivyo ipandishwe daraja na kuwa barabara ya mkoa chini ya TANROADS.

Mheshimiwa Spika, TARURA kwa kushirikiana na Bodi ya Barabara ya Mkoa itaanzisha mchakato wa kuzipandisha hadhi barabara hizo katika mwaka 2025/2026 ili ziweze kuwa chini ya TANROADS.