Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 330 2025-05-16

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:-

Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Namwanga baada ya Halmashauri ya Masasi kuanza ujenzi huo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Namwanga kinajengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Masasi ambapo kimeanza na ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD), mpaka sasa Halmashauri ya Masasi imetoa shilingi milioni 100 na ujenzi upo katika hatua ya ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Masasi imetenga shilingi milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na Serikali Kuu itapeleka fedha za ujenzi wa majengo mengine katika Kituo cha Afya cha Namwanga, ahsante. (Makofi)