Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 35 2026-04-08

Name

Dickson Nathan Lutevele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DICKSON N. LUTEVELE aliuliza: -

Je, lini malipo ya waliokuwa wafanyakazi wa Kiwanda cha Karatasi (SPM Mgololo) yatafanyika, ukizingatia kuwa ni ya muda mrefu sana?

Name

Denis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara ninaomba nijibu swali namba 35 kutoka kwa Mheshimiwa Dickson Nathan Lutevele, Mbunge wa Mafinga Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Southern Paper Mills Ltd. (SPM) ilibinafsishwa mwezi Februari, 2004 kwa mwekezaji aitwae RAI Group kutoka Kenya. Baada ya ubinafsishwaji, wafanyakazi wapatao 760 wa kiwanda hicho walifungua Shauri Na.162/2017 la madai katika Mahakama Kuu Tanzania Divisheni ya Kazi dhidi ya Serikali wakidai mafao ya utumishi wao kabla ya kubinafsisha kiwanda hicho. Suala hili la madai ya wafanyakazi hawa bado lipo ngazi ya Mahakama.