Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 34 | 2026-04-08 |
Name
Catherine Canute Joachim
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CATHERINE C. JOACHIM aliuliza: -
Je, kuna mpango gani wa kuendeleza utalii wa tiba nchini ili kuboresha huduma za afya na kuongeza mchango wa sekta ya afya katika pato la Taifa?
Name
Dr. Florence George Samizi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Joachim, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuendeleza utalii wa tiba nchini Serikali inatekeleza mpango wa uboreshaji wa huduma za ubingwa na ubingwa bobezi wenye vipaumbele vifuatavyo; uboreshaji wa miundombinu kwa kujenga mipya na kukarabati iliyochakaa, kuboresha upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa (PET/CT Scan, Angio Suite, Cathlab na CT Scan), kuwajengea uwezo watumishi katika utoaji wa huduma kwa kuwaendeleza kitaaluma, kuanzisha huduma mpya za ubingwa bobezi, kuziwezesha hospitali zetu kupata ithibati za kimataifa na kuzitangaza huduma zinazotolewa na hospitali hizo nchi za nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha Julai, 2025 hadi Februari, 2026 jumla ya wagonjwa 3,018 raia wa kigeni walipatiwa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi katika Hospitali za Rufaa za Mkoa, Kanda, Hospitali Maalum Taifa, hivyo kuongeza mchango wa sekta ya afya katika ukuzaji wa pato la Taifa. Aidha, Serikali imetoa ufadhili wa masomo wa Samia Health Super-Specialization Program ambapo jumla ya wataalam 1,483 wanafadhiliwa kusomea fani za ubingwa na ubingwa bobezi katika nchi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved