Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 34 2026-04-08

Name

Catherine Canute Joachim

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CATHERINE C. JOACHIM aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuendeleza utalii wa tiba nchini ili kuboresha huduma za afya na kuongeza mchango wa sekta ya afya katika pato la Taifa?

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Joachim, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuendeleza utalii wa tiba nchini Serikali inatekeleza mpango wa uboreshaji wa huduma za ubingwa na ubingwa bobezi wenye vipaumbele vifuatavyo; uboreshaji wa miundombinu kwa kujenga mipya na kukarabati iliyochakaa, kuboresha upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa (PET/CT Scan, Angio Suite, Cathlab na CT Scan), kuwajengea uwezo watumishi katika utoaji wa huduma kwa kuwaendeleza kitaaluma, kuanzisha huduma mpya za ubingwa bobezi, kuziwezesha hospitali zetu kupata ithibati za kimataifa na kuzitangaza huduma zinazotolewa na hospitali hizo nchi za nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha Julai, 2025 hadi Februari, 2026 jumla ya wagonjwa 3,018 raia wa kigeni walipatiwa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi katika Hospitali za Rufaa za Mkoa, Kanda, Hospitali Maalum Taifa, hivyo kuongeza mchango wa sekta ya afya katika ukuzaji wa pato la Taifa. Aidha, Serikali imetoa ufadhili wa masomo wa Samia Health Super-Specialization Program ambapo jumla ya wataalam 1,483 wanafadhiliwa kusomea fani za ubingwa na ubingwa bobezi katika nchi mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)