Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 31 2026-04-08

Name

Ester Edwin Malleko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa hoteli katika Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha uandaaji wa pembuzi yakinifu ya ujenzi wa Hoteli ya Nyota Nne katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro. Kwa sasa taratibu za kutafuta mwekezaji wa ujenzi wa hoteli zinaendelea.