Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 30 2026-04-08

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIGRADA W. MLIGO K.n.y. MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa bandari ndogo ya Kagunga na Soko la Kagunga utakamilika ili kuimarisha biashara kati ya Tanzania na Burundi?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamimzi wa Bandari Tanzania (TPA) mnamo mwaka 2015 ilitekeleza mradi wa upanuzi wa Bandari ya Kagunga wenye thamani ya shilingi bilioni 3.8, uliohusisha ujenzi wa gati, ghala la mizigo, jengo la abiria, nyumba ya wafanyakazi, vyoo, uzio na kibanda cha mlinzi. Mradi huu ulikamilika mwezi Januari, 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali pia kupitia TPA iliingia Mkataba na Mkandarasi ESSAU Construction Ltd. wenye thamani ya shilingi milioni 190.2 kwa mfumo wa Kurudisha kwa Jamii au Corporate Social Responsibility (CSR) kwa Halmashauri ya Kigoma Vijijini kwa ajili ya ujenzi wa soko ambao nao umekamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kutokana na mabadiliko ya tabianchi yaliyopelekea maji kujaa, bandari hii kwa sasa haitumiki. Serikali kupitia TPA inaendelea na mpango wa kufanya maboresho ya bandari hiyo na hatua iliyofikiwa ni kufanya utafiti wa namna bora ya kutatua changamoto ya kujaa kwa maji na maboresho jumla ya bandari hiyo.