Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 30 | 2026-04-08 |
Name
Kiza Hussein Mayeye
Sex
Female
Party
CUF
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SIGRADA W. MLIGO K.n.y. MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa bandari ndogo ya Kagunga na Soko la Kagunga utakamilika ili kuimarisha biashara kati ya Tanzania na Burundi?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamimzi wa Bandari Tanzania (TPA) mnamo mwaka 2015 ilitekeleza mradi wa upanuzi wa Bandari ya Kagunga wenye thamani ya shilingi bilioni 3.8, uliohusisha ujenzi wa gati, ghala la mizigo, jengo la abiria, nyumba ya wafanyakazi, vyoo, uzio na kibanda cha mlinzi. Mradi huu ulikamilika mwezi Januari, 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali pia kupitia TPA iliingia Mkataba na Mkandarasi ESSAU Construction Ltd. wenye thamani ya shilingi milioni 190.2 kwa mfumo wa Kurudisha kwa Jamii au Corporate Social Responsibility (CSR) kwa Halmashauri ya Kigoma Vijijini kwa ajili ya ujenzi wa soko ambao nao umekamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kutokana na mabadiliko ya tabianchi yaliyopelekea maji kujaa, bandari hii kwa sasa haitumiki. Serikali kupitia TPA inaendelea na mpango wa kufanya maboresho ya bandari hiyo na hatua iliyofikiwa ni kufanya utafiti wa namna bora ya kutatua changamoto ya kujaa kwa maji na maboresho jumla ya bandari hiyo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved