Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 28 | 2026-04-08 |
Name
Twaha Said Mwakioja
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Primary Question
MHE. TWAHA S. MWAKIOJA aliuliza: -
Je, lini Serikali itawapatia maji safi na salama wananchi wa Wilaya ya Mkinga kupitia Mradi wa Tanga – Horohoro?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Said Mwakioja, Mbunge wa Jimbo la Mkinga kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji Mkinga – Horohoro kwa gharama ya shilingi bilioni 35.4. Kazi zinazotekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa matanki 10 yenye jumla ya ujazo wa lita 2,450,000, ulazaji wa mabomba yenye umbali wa kilometa 223.7 sanjari na ujenzi wa vituo 58 vya kuchotea maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi wa Mkinga – Horohoro umefikia wastani wa 65% na umeanza kutoa huduma kwa wananchi wa Kijiji cha Mtimbwani. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2026 na kunufaisha wananchi wapatao 57,334 waishio katika vijiji 37 katika Wilaya ya Mkinga, mkoani Tanga.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved