Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 28 2026-04-08

Name

Twaha Said Mwakioja

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. TWAHA S. MWAKIOJA aliuliza: -

Je, lini Serikali itawapatia maji safi na salama wananchi wa Wilaya ya Mkinga kupitia Mradi wa Tanga – Horohoro?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Said Mwakioja, Mbunge wa Jimbo la Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji Mkinga – Horohoro kwa gharama ya shilingi bilioni 35.4. Kazi zinazotekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa matanki 10 yenye jumla ya ujazo wa lita 2,450,000, ulazaji wa mabomba yenye umbali wa kilometa 223.7 sanjari na ujenzi wa vituo 58 vya kuchotea maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi wa Mkinga – Horohoro umefikia wastani wa 65% na umeanza kutoa huduma kwa wananchi wa Kijiji cha Mtimbwani. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2026 na kunufaisha wananchi wapatao 57,334 waishio katika vijiji 37 katika Wilaya ya Mkinga, mkoani Tanga.