Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 26 2026-04-08

Name

Alan Thomas Mvano

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kakonko

Primary Question

MHE. ALAN T. MVANO aliuliza: -

Je, lini Barabara ya Kakonko kwenda mpaka wa Muhange kupitia Gwarama kilometa 41.43 itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Alan Thomas Mvano, Mbunge wa Kakonko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Kakonko – Gwarama – Muhange yenye urefu wa kilometa 41.43 ni barabara kuu inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Kigoma. Kwa sasa Serikali ipo katika hatua ya kutafuta fedha ili kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, ikiwa ni hatua ya awali katika mchakato wa kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, usanifu utakapokamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)