Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 26 | 2026-04-08 |
Name
Alan Thomas Mvano
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kakonko
Primary Question
MHE. ALAN T. MVANO aliuliza: -
Je, lini Barabara ya Kakonko kwenda mpaka wa Muhange kupitia Gwarama kilometa 41.43 itajengwa kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Alan Thomas Mvano, Mbunge wa Kakonko, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Kakonko – Gwarama – Muhange yenye urefu wa kilometa 41.43 ni barabara kuu inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Kigoma. Kwa sasa Serikali ipo katika hatua ya kutafuta fedha ili kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, ikiwa ni hatua ya awali katika mchakato wa kuijenga kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usanifu utakapokamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved