Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 4 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 23 | 2026-04-08 |
Name
Devotha Daniel Mburarugaba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DEVOTHA D. MBURARUGABA aliuliza:-
Je, hatua gani inachukuliwa kuhakikisha usimamizi, utoaji, urejeshaji wa mikopo 10% ya halmashauri unakuwa wazi na unawafikia walengwa?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Daniel Mburarugaba, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Kagera kuwa Serikali imeweka utaratibu wa kuhakikisha mchakato mzima wa usimamizi, utoaji na urejeshaji wa mikopo unakuwa wa uwazi na usawa. Utaraibu huo umeainishwa kwenye kanuni na katika mwongozo ambao halmashauri zote nchini zimepatiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kanuni, mwongozo pamoja na vitini vya mafunzo vinaelekeza halmashauri baada ya kukusanya fedha kwa ajili ya mikopo zinapaswa kutoa tangazo kwa njia mbalimbali ili kuufahamisha umma. Sambamba na hilo Serikali imeunda mfumo wa kielektroniki wa utoaji na usimamizi wa mikopo ambapo kila mwombaji anautumia kuomba mkopo. Mfumo huu unatumika pia katika usimamizi wa shughuli za vikundi pamoja na kufuatilia marejesho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua hii imesaidia kuweka wazi uwajibikaji katika kila hatua ya utoaji wa mikopo, usimamizi na marejesho. Serikali itaendelea kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa kunakuwa na uwazi katika uombaji na utoaji wa mikopo, kama kanuni na miongozo inavyoelekeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved