Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 104 | 2026-02-03 |
Name
Suma Ikenda Fyandomo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -
Je, lini Kiwanda cha Chai cha WATCO kilichopo Katumba – Tukuyu Wilaya ya Rungwe, kitafunguliwa?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imefanya jitihada za kuhakikisha Kiwanda cha Chai cha WATCO kinafunguliwa ambapo Kampuni ya WATCO inayosimamia kiwanda hicho imepata mkopo ambao umetumika kulipa madai ya wakulima, wafanyakazi na watoa huduma wengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya malipo hayo, hatua inayofuata ni ufunguzi wa kiwanda hicho ambacho kinatarajiwa kufunguliwa ifikapo tarehe 2 Machi, 2026 baada ya kukamilika kwa usafi na ukarabati. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved