Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 99 2026-02-03

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Iguguno - Nduguti - Sibiti (kilometa 89) na Barabara unganishi za daraja la Mto Sibiti (kilometa 24.83)?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza mipango ya ujenzi wa Barabara ya Iguguno – Nduguti – Sibiti yenye urefu wa kilometa 84.95 ambapo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Ili kurahisisha utekelezaji wa mradi huu, Serikali imepanga kuijenga kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa barabara unganishi za Daraja la Mto Sibiti, Mkandarasi amepatikana, na taratibu za kuanza kazi za ujenzi zinaendelea. Aidha, Serikali inaendelea na taratibu za manunuzi ya kumpata mkandarasi, kwa ajili ya ujenzi wa Sehemu ya Nduguti Mjini yenye urefu wa kilometa 10. Baada ya hatua za manunuzi kukamilika na mkandarasi kupatikana, kazi za ujenzi zitaanza, ahsante.