Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 98 2026-02-03

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, lini Uwanja wa Ndege wa Kyabajwa utaanza kujengwa?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza kutekeleza Mradi wa Kiwanja Kipya cha Mkoa wa Kagera kwa kuingia mkataba na mtaalamu elekezi, ili kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa kiwanja hicho kinachotarajiwa kujengwa katika Eneo la Kyabajwa. Mtaalamu elekezi anatarajiwa kukabidhiwa eneo la kazi na kuanza kazi ndani ya robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026 (Januari – Machi, 2026).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imepangwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2026. Baada ya hapo, hatua za utekelezaji wa mradi huo zitaanza.