Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 98 | 2026-02-03 |
Name
Florent Laurent Kyombo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkenge
Primary Question
MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -
Je, lini Uwanja wa Ndege wa Kyabajwa utaanza kujengwa?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza kutekeleza Mradi wa Kiwanja Kipya cha Mkoa wa Kagera kwa kuingia mkataba na mtaalamu elekezi, ili kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa kiwanja hicho kinachotarajiwa kujengwa katika Eneo la Kyabajwa. Mtaalamu elekezi anatarajiwa kukabidhiwa eneo la kazi na kuanza kazi ndani ya robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026 (Januari – Machi, 2026).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imepangwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2026. Baada ya hapo, hatua za utekelezaji wa mradi huo zitaanza.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved