Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 97 | 2026-02-03 |
Name
Kiza Hussein Mayeye
Sex
Female
Party
CUF
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza: -
Je, Serikali imechukua hatua gani za kurejesha Bandari za Kibirizi na Ujiji zilizokumbwa na madhara ya Mabadiliko ya Tabianchi na kujaa maji?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TPA imefanya tathmini ya madhara yaliyosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi, hususan kuongezeka kwa vina vya maji katika Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa ambapo baadhi ya Bandari kama Ujiji na Kibirizi zimeathirika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa TPA imeanza kazi za ukarabati na kuweka miundombinu mbadala, ili Bandari hizo za Kibirizi na Ujiji zirejee kufanya kazi kama ilivyokuwa awali. Aidha, kazi zinazoendelea zinatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Juni, 2026.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved