Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 97 2026-02-03

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza: -

Je, Serikali imechukua hatua gani za kurejesha Bandari za Kibirizi na Ujiji zilizokumbwa na madhara ya Mabadiliko ya Tabianchi na kujaa maji?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TPA imefanya tathmini ya madhara yaliyosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi, hususan kuongezeka kwa vina vya maji katika Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa ambapo baadhi ya Bandari kama Ujiji na Kibirizi zimeathirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa TPA imeanza kazi za ukarabati na kuweka miundombinu mbadala, ili Bandari hizo za Kibirizi na Ujiji zirejee kufanya kazi kama ilivyokuwa awali. Aidha, kazi zinazoendelea zinatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Juni, 2026.