Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 6 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 95 | 2026-02-03 |
Name
Dr. Wilson Charles Mahera
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Butiama
Primary Question
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza maji Kata za Bisumwa, Bukabwa, Nyankanga, Butuguri, Bwiregi, Buruma, Kyanyari, Buhemba, Mirwa na Kikirango?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Wilson Mahera Charles, Mbunge wa Jimbo la Butiama, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha ujenzi wa Mradi mkubwa wa Maji ya Ziwa Victoria wa Mugango – Kiabakari - Butiama uliogharimu zaidi ya shilingi bilioni 70 na unanufaisha wananchi kwenye Kata za Wilaya za Butiama na baadhi ya maeneo ya Wilaya za Bunda pamoja na Musoma Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa mradi huo umeanza kutoa huduma kwenye vijiji 22 vinavyopatikana kwenye kata saba za Wilaya za Butiama na Musoma Vijijini. Aidha, kazi ya upanuzi wa mradi huo inaendelea kwa awamu kadiri fedha zinavyopatikana ili kuweza kufikisha huduma ya majisafi na salama kwenye maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo ikiwemo baadhi ya vijiji vya Kata za Bisumwa, Bukabwa, Nyankanga, Butuguri, Bwiregi, Buruma, Kyanyari, Buhemba, Mirwa pamoja na Kikirango.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved