Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 93 2026-02-03

Name

Patrick Adkin Mwalunenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. PATRICK A. MWALUNENGE aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha Mradi mkubwa wa Maji kutoka chanzo cha Mto Kiwira ili kukomesha tatizo la maji Mbeya Mjini?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Patrick Mwalunenge, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa kutoa maji Mto Kiwira kwenda Jijini Mbeya. Miongoni mwa kazi zinazotekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake) na mtambo wa kutibu maji lita milioni 117 kwa siku, ujenzi wa matanki mawili yenye uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni 10 sambamba na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 37.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 48% na kwa mujibu wa mkataba unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2026 ambapo utanufaisha zaidi ya wakazi 890,000 wa Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi. (Makofi)