Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 2 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 39 | 2026-01-28 |
Name
Onesmo Merdson Mnkondya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbozi
Primary Question
MHE. ONESMO M. MNKONDYA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha mbolea inapatikana kwa haraka wakati wa msimu wa kilimo?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Onesmo Merdson Mnkondya, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakati kwa wakulima. Mikakati hiyo ni pamoja na kuandaa mahitaji kwa wakati, kuhusisha vyama vya ushirika kusambaza mbolea na kuhamasisha kampuni za mbolea na mawakala binafsi kufungua vituo vya mauzo ya mbolea kwenye maeneo ya uzalishaji.
Mheshimiwa Spika, kutokana na jitihada hizo, Kampuni za mbolea za OCP, METL, ETG Inputs Limited, ITRACOM, MINJINGU, One Acre Fund, Premium Limited, na AFRISIAN zimefungua ghala nane za mbolea katika Wilaya ya Mbozi na kusajili mawakala 174 ili kusambaza mbolea kwenye jumla ya vituo vya mauzo 85 katika wilaya hiyo. Lengo ni kuhakikisha mbolea zinapatikana kwa wakati ili wakulima waweze kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved