Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 39 2026-01-28

Name

Onesmo Merdson Mnkondya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ONESMO M. MNKONDYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha mbolea inapatikana kwa haraka wakati wa msimu wa kilimo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Onesmo Merdson Mnkondya, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakati kwa wakulima. Mikakati hiyo ni pamoja na kuandaa mahitaji kwa wakati, kuhusisha vyama vya ushirika kusambaza mbolea na kuhamasisha kampuni za mbolea na mawakala binafsi kufungua vituo vya mauzo ya mbolea kwenye maeneo ya uzalishaji.

Mheshimiwa Spika, kutokana na jitihada hizo, Kampuni za mbolea za OCP, METL, ETG Inputs Limited, ITRACOM, MINJINGU, One Acre Fund, Premium Limited, na AFRISIAN zimefungua ghala nane za mbolea katika Wilaya ya Mbozi na kusajili mawakala 174 ili kusambaza mbolea kwenye jumla ya vituo vya mauzo 85 katika wilaya hiyo. Lengo ni kuhakikisha mbolea zinapatikana kwa wakati ili wakulima waweze kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo.