Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 37 2026-01-28

Name

John Stephano Luhende

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. JOHN S. LUHENDE aliuliza:-

Je, lini usajili wa Bodi ya Wanajiolojia nchini utakamilika ili kulinda na kuongeza ufanisi katika shughuli za utafiti na uchimbaji madini?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa John Stephano Luhende, Mbunge wa Bukene kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na hatua za uanzishwaji wa Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Jiosayansi Tanzania (Tanzania Geoscientists Registration Board), kwa kifupi itajulikana kama (TGRB). Taratibu ambazo zimeshatekelezwa ni pamoja na uandaaji wa rasimu ya Waraka wa Mapendekezo ya Baraza la Mawaziri, kuhusu kuanzishwa kwa bodi hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa, Wizara ya Madini ipo katika hatua ya ukusanyaji wa maoni na mapendekezo kutoka kwa wadau kuhusu masuala mbalimbali likiwemo suala la kuainishwa kwa vyanzo vya mapato vitakavyohakikisha bodi pendekezwa inaweza kujiendesha.

Mheshimiwa Spika, baada ya zoezi la ukusanyaji na uchambuzi wa maoni kutoka kwa wadau kukamilika, Wizara itawasilisha waraka huo kwenye ngazi za maamuzi za Serikali ikiwa ni pamoja na ngazi ya kikao cha kitaalamu cha Makatibu Wakuu (IMTC) na kikao cha Baraza la Mawaziri kwa ajili ya kujadiliwa na kupata ridhaa ya kuanzishwa rasmi kwa bodi hiyo kwa mujibu wa sheria. Ahsante sana.