Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 2 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 36 | 2026-01-28 |
Name
Boniphace Mwita Getere
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda
Primary Question
MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:-
Je, lini Wananchi walioharibiwa mazao yao na Tembo katika Vijiji vya Jimbo la Bunda watalipwa kifuta jasho?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Wizara ililipa kifuta jasho na machozi jumla ya shilingi 311,160,000 kwa wananchi 1,115 wa Wilaya ya Bunda. Aidha, Wizara imekamilisha uchambuzi wa madai ya kifuta jasho na machozi ambapo shilingi 524,122,500 kwa wananchi 1,603 wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda zitalipwa. Kwa sasa Wizara inakamilisha taratibu za malipo hayo ili wananchi husika walipwe stahiki zao kwa mujibu wa Kanuni kupitia mfumo wa kieletroniki ujulikanao kwa jina la Problem Animal Information System – (PAIS).
Mheshimiwa Spika, sambamba na mfumo huu mpya kwa sasa, Serikali itaendelea kulipa wananchi ambao hawana account au namba za siku kwa kutumia utaratibu wa awali ambapo wataalamu hufika uwandani kufanya malipo hayo. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved