Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 34 2026-01-28

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. KANGI A. LUGOLA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Mradi mkubwa wa Maji katika Jimbo la Mwibara utaanza?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda vijiji 30 vya Jimbo la Mwibara Wilayani Bunda. Miongoni mwa kazi zinazotarajiwa kutekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake) na mtambo wa kutibu maji (treatment plant) mwenye kuzalisha lita milioni 35.7, ujenzi wa nyumba ya mitambo (booster station), ujenzi wa matanki 10 yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 19.3, ulazaji wa mtandao wa bomba zaidi ya umbali wa kilometa 500, ujenzi wa mbauti 30 za kunyweshea mifugo, ujenzi wa vituo 124 vya kuchotea maji sanjari na maunganisho kwa wateja 5,000 wa majumbani.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuanza utekelezaji wa mradi huo unaotarajia kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 94 ambapo utanufaisha zaidi ya wananchi 200,000 wa Jimbo la Mwibara.