Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 2 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 33 | 2026-01-28 |
Name
Prof. Joyce Lazaro Ndalichako
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kasulu Mjini
Primary Question
MHE. PROF. JOYCE L. NDALICHAKO aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza utekelezaji wa Mradi wa Usambazaji wa Maji wa Mwanga B – Kasulu?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa mradi wa maji Mwanga B uliopo Mji wa Kasulu mkoani Kigoma ambapo hadi sasa Mkandarasi ameshapeleka mabomba yote ya mradi yenye urefu wa jumla ya kilometa 52 eneo la mradi. Kazi nyingine zinazotarajiwa kutekelezwa katika mradi huo ni pamoja na kubadili mfumo wa nishati ya umeme wa jua kwenda umeme wa gridi kwa ajili ya uzalishaji maji sambamba na ujenzi wa chemba za ukaguzi wa mitambo ya mabomba.
Mheshimiwa Spika, Serikali inahakikisha inapeleka fedha za utekelezaji wa mradi huo ili uweze kukamilika na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi waishio katika mitaa sita ya Mwanga B, Mganza, Msambala, Nyachidima, Kimombwa na Kigondo, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved