Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 32 2026-01-28

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka Maji ya mserereko katika Kijiji cha Kapalala Kata ya Kapalala - Nsimbo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya upungufu wa maji kwa wananchi wa Kijiji cha Kapalala Kata ya Kapalala kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Wilayani Mpanda. Kijiji hicho kwa sasa kinapata huduma ya maji kupitia visima vitatu vyenye uwezo wa kuzalisha maji lita 23,742 kwa siku wakati mahitaji ya wananchi wa kijiji hicho ni lita 72,675 kwa siku.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali imekamilisha usanifu wa kina wa mradi wa kutumia chanzo cha maji ya mserereko cha Ikolongo ambapo unatarajia kunufaisha vijiji tisa Wilayani Mpanda kikiwemo Kijiji cha Kapalala. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha za utekelezaji wa mradi huo unaotarajia kugharimu takribani shilingi bilioni saba.

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru.