Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 29 2026-01-28

Name

Kakulu Burchard Kakulu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. KAKULU B. KAKULU aliuliza: -

Je, lini upanuzi wa Barabara ya Kilwa kuanzia Mbagala Rangi Tatu – Kongowe unatarajiwa kukamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) iliingia mkataba na Mkandarasi M/S STECOL Corporation kwa ajili ya upanuzi wa Barabara ya Kilwa kuanzia Mbagala Rangi Tatu – Kongowe yenye urefu wa kilometa 3.8. Mkataba ulisainiwa tarehe 19 Agosti, 2025 na utatekelezwa kwa muda wa miezi 15. Kazi za ujenzi zinatarajiwa kukamilika mwezi Novemba mwaka huu 2026.