Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 28 2026-01-28

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza: -

Je, ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kibaha Maili Moja hadi Chalinze umefikia katika hatua gani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Barabara ya kutoka Kibaha Maili Moja hadi Chalinze umegawanywa katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ya kutoka Maili Moja – Picha ya Ndege yenye urefu wa kilometa 3.6 kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya upanuzi wa sehemu hiyo ipo katika hatua za mwisho. Usanifu utakapokamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Spika, sehemu iliyobaki ya kutoka Picha ya Ndege – Chalinze yenye urefu wa kilometa 78.9 itatekelezwa kwa njia ya ubia kati ya Serikali na sekta binafsi (PPP). Kwa sasa taratibu za manunuzi ya kumpata mbia zinaendelea.