Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 2 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 25 2026-01-28

Name

Ester Edwin Malleko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha fedha za TASAF zinawafikia walengwa?

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu. Kipekee nimshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani yake kubwa kwangu kwa kuniamini na kuniteua kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Ahadi yangu kwake ni kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kujituma, na kwa uzalendo, ili malengo yaliyopangwa yafikiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, sasa naomba nijibu swali la Mheshimiwa Esther Malleko, Mbunge wa Viti Maalum.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia program ya TASAF, imeweka mkakati mahususi wa kuhakikisha fedha/ruzuku zinawafikia walengwa kupitia matumizi ya mfumo wa malipo ya kielektroniki (e-payments) unaolenga kuongeza uwazi, usalama na ufanisi katika utoaji wa ruzuku kwa walengwa. Mkakati huo unatekelezwa kwa kutumia watoa huduma za kifedha walioidhinishwa ambao hulipa fedha moja kwa moja kwenda kwa walengwa kupitia akaunti zao za benki na mitandao ya simu.

Mheshimiwa Spika, mfumo huu huondoa utaratibu wa kutuma fedha taslimu, na hivyo kupunguza mianya ya upotevu, ucheleweshaji au matumizi yasiyo sahihi ya fedha. Pili, malipo yote hufanyika kwa kuzingatia taarifa za walengwa zilizohakikiwa katika mfumo wa usimamizi wa walengwa, Management Information System (MIS), ambapo kila mlengwa hulipwa kulingana na utambulisho wake wa kipekee, ahsante.