Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 2 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 21 | 2026-01-28 |
Name
Fadhili Fabian Ngajilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Iringa Mjini
Primary Question
MHE. FADHILI F. NGAJILO aliuliza:-
Je, lini Daraja la Isakalilo – Kitwiru litajengwa, ili kufungua Utalii wa Mbuga ya Wanyama Ruaha?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Fadhili Fabian Ngajilo, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Daraja la Isakalilo – Kitwiru lipo katika Barabara ya Isakalilo – Kitwiru yenye urefu wa kilomita tatu, ambayo inaunganisha kati ya Barabara ya TANZAM na Iringa kwenda Msembe. Daraja hili ni kiunganishi muhimu kuifikia Mbuga ya Wanyama ya Ruaha.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mradi wa TACTIC, Awamu ya Pili, imefanya usanifu wa mradi. Baada ya kukamilika kwa usanifu, mradi huu unaojumuisha ujenzi wa daraja pamoja na barabara za maingilio zenye urefu wa kilomita taru utaanza kutekelezwa.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved